Saturday , 4 May 2024
Home Kitengo Michezo Ibenge: Siwezi kuogopa, tumekuja kucheza
Michezo

Ibenge: Siwezi kuogopa, tumekuja kucheza

Spread the love

KOCHA wa klabu ya As Vita Florent Ibenge amesema hawezi kuhofia wala kuogopa kucheza na Simba kutokana na ubora waliokuwa nao kwa sasa na wao wamekuja kucheza mpira. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Mchezo huo wa kundi J, utapigwa kesho majira ya saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa kesho Ibenge amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya Simba na wamekuja kucheza wala haogopi kucheza dhidi ya Simba bali anafurahi kucheza nao.

“Tunapenda mpira na tunapenda kuucheza, tumefanya kazi kubwa kuja kucheza dhidi ya Simba ambayo ni timu bora kwa sasa Afrika.

“Siogopi kucheza dhidi ya Simba ila nafurahia kucheza nao na tunataka kufurahia mchezo. Tukipoteza kesho tumetoka, kwa hiyo tumejipanga kuhakikisha tunapata matokeo”, amesema Ibenge.

Katika mchezo wa kwanza waliocheza nchini Jamhuri ya Congo, Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0.

Kwa upande wa mlinda mlango wa klabu hiyo Nathan, amesema wamekuja nchini Tanzania kwa aajili ya kucheza, walipoteza kwenye mchezo uliopita kutokana na kutocheza kama walivyotaka wao.

“Tulipoteza mchezo wa kwanza Kinshasa kwa sababu hatukucheza kama tulivyotaka, tumekuja Tanzania kwa ajili ya mechi ambayo tukishinda tutajiweka sehemu nzuri kwa ajili ya kufuzu hatua inayofuata.

“Mechi haitakuwa rahisi lakini kama Simba iliweza kushinda kwetu kwa nini sisi tushindwe kushinda kwao? Tutajitoa kwa ajili ya kupata ushindi”. Amesema kipa huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

error: Content is protected !!