Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo: Tutashiriki uchaguzi Muhambwe
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo: Tutashiriki uchaguzi Muhambwe

Spread the love

CHAMA cha siasa cha ACT-Wazalendo nchini Tanzania, kimesema kinakwenda kushiriki na kushinda uchaguzi mdogo wa ubunge wa Muhambwe, mkoani Kigoma utakaofanyika tarehe 2 Mei 2021.

Uchaguzi huo, unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge wake kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Atashasta Nditiye kufariki dunia tarehe 12 Februari 2021, kwa ajili ya gari, iliyotokea jijini Dodoma.

Fomu za kuomba kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), zimeanza kutolewa kuanzia tarehe 28 Machi hadi 3 Aprili, kisha uteuzi utafanyika na kampeni kuanzia hadi 1 Mei 2021.

MwanaHALISI TV, limefanya mahojiano maalum na Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu kuhusu maandalizi ya uchaguzi huo, ujumbe wao kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, wananchi watarajie kampeni za aina gani.

Ado amegusia uchaguzi huu ambao ni wa kwanza kwa Rais Samia Suluhu Hassan kufanyika tangu alipoingia madarakani tarehe 19 Machi 2021, wakimpa tahadhari ya kuchukua. Amejinasibu juu ya mgombea wao na yule wa Chama Cha Mapinduzi, Dk. Florence Samizi.

Fuatilia mahojiano yake na MwanaHALISI TV

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!