Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mpango kuapishwa kesho Ikulu-Dodoma
Habari za Siasa

Dk. Mpango kuapishwa kesho Ikulu-Dodoma

Dk. Philip Mpango, Makamu wa Rais Tanzania
Spread the love

 

DAKTARI Philip Isdor Mpango, kesho Jumatano tarehe 31 Machi 2021, saa 9:00 alasiri, ataapishwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Dk. Mpango, aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mipango, anaapishwa baada ya kupendelezwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kuwa makamu wa Rais.

Rais Samia amewasilisha jina la Dk. Mpango leo Jumanne tarehe 30 Machi 2021, bungeni kupitia kwa mapambe wale na Bunge limemthibitisha kwa kura zote za wabunge 363 waliohudhuria sawa na asilimia 100.

Mara baada ya Bunge kumthitibisha, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa amesema, hafla ya kuapishwa kwa Dkt. Mpango mwenye miaka 63 itafanyika Ikulu, Chamwino mkoani Dodoma.

Msigwa amesema, Dk. Mpango ataapishwa kushika wadhifa huo baada ya Rais Samia, kuwasilisha mapendekezo ya jina lake kuwa Makamu wa Rais katika Kikao Maalum cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!