Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mpango kuapishwa kesho Ikulu-Dodoma
Habari za Siasa

Dk. Mpango kuapishwa kesho Ikulu-Dodoma

Dk. Philip Mpango, Makamu wa Rais Tanzania
Spread the love

 

DAKTARI Philip Isdor Mpango, kesho Jumatano tarehe 31 Machi 2021, saa 9:00 alasiri, ataapishwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Dk. Mpango, aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mipango, anaapishwa baada ya kupendelezwa na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kuwa makamu wa Rais.

Rais Samia amewasilisha jina la Dk. Mpango leo Jumanne tarehe 30 Machi 2021, bungeni kupitia kwa mapambe wale na Bunge limemthibitisha kwa kura zote za wabunge 363 waliohudhuria sawa na asilimia 100.

Mara baada ya Bunge kumthitibisha, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa amesema, hafla ya kuapishwa kwa Dkt. Mpango mwenye miaka 63 itafanyika Ikulu, Chamwino mkoani Dodoma.

Msigwa amesema, Dk. Mpango ataapishwa kushika wadhifa huo baada ya Rais Samia, kuwasilisha mapendekezo ya jina lake kuwa Makamu wa Rais katika Kikao Maalum cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!