Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Michezo Samatta amlilia Rais Magufuli
Michezo

Samatta amlilia Rais Magufuli

Rais John Magufuli
Spread the love

 

NAHODHA wa timu ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Mbwana Samatta amewaomba wananchi, kushikamana katika kipindi hiki cha majonzi ya kumpoteza, Rais John Pombe Magufuli (61). Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea)

Samatta anayekipiga katika klabu ya Fenerbahçe ya Uturuki, ametoa ombi hilo leo Alhamisi tarehe 18 Machi 2021, kupitia akaunti yake ya Twitter.

Nasaha hizo, amezitoa saa chache kupita, tangu Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, alipotangaza kifo cha Rais Magufuli, aliyefariki jana Jumatano saa 12:00 jioni, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu ya moyo.

Samatta ameandika “Tutakukumbuka daima milele mzee wetu, umeumaliza mwendo tunaomba kwa mungu upumzike kwa amani.”

“R.i.p Mr president 🙏🏿🙏🏿 umetuachia simanzi na majonzi. Poleni wanafamilia wa mpendwa wetu poleni watanzania wenzangu. Tuendelee kushikamana katika kipindi hiki cha majonzi,” amesema Samatta, mchezaji wa zamani wa Aston Villa ya Uingereza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!