Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Samatta amlilia Rais Magufuli
Michezo

Samatta amlilia Rais Magufuli

Rais John Magufuli
Spread the love

 

NAHODHA wa timu ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Mbwana Samatta amewaomba wananchi, kushikamana katika kipindi hiki cha majonzi ya kumpoteza, Rais John Pombe Magufuli (61). Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea)

Samatta anayekipiga katika klabu ya Fenerbahรงe ya Uturuki, ametoa ombi hilo leo Alhamisi tarehe 18 Machi 2021, kupitia akaunti yake ya Twitter.

Nasaha hizo, amezitoa saa chache kupita, tangu Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, alipotangaza kifo cha Rais Magufuli, aliyefariki jana Jumatano saa 12:00 jioni, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu ya moyo.

Samatta ameandika “Tutakukumbuka daima milele mzee wetu, umeumaliza mwendo tunaomba kwa mungu upumzike kwa amani.”

“R.i.p Mr president ๐Ÿ™๐Ÿฟ๐Ÿ™๐Ÿฟ umetuachia simanzi na majonzi. Poleni wanafamilia wa mpendwa wetu poleni watanzania wenzangu. Tuendelee kushikamana katika kipindi hiki cha majonzi,” amesema Samatta, mchezaji wa zamani wa Aston Villa ya Uingereza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!