Tuesday , 21 March 2023
Home Kitengo Michezo Samatta amlilia Rais Magufuli
Michezo

Samatta amlilia Rais Magufuli

Rais John Magufuli
Spread the love

 

NAHODHA wa timu ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Mbwana Samatta amewaomba wananchi, kushikamana katika kipindi hiki cha majonzi ya kumpoteza, Rais John Pombe Magufuli (61). Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea)

Samatta anayekipiga katika klabu ya Fenerbahรงe ya Uturuki, ametoa ombi hilo leo Alhamisi tarehe 18 Machi 2021, kupitia akaunti yake ya Twitter.

Nasaha hizo, amezitoa saa chache kupita, tangu Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, alipotangaza kifo cha Rais Magufuli, aliyefariki jana Jumatano saa 12:00 jioni, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu ya moyo.

Samatta ameandika “Tutakukumbuka daima milele mzee wetu, umeumaliza mwendo tunaomba kwa mungu upumzike kwa amani.”

“R.i.p Mr president ๐Ÿ™๐Ÿฟ๐Ÿ™๐Ÿฟ umetuachia simanzi na majonzi. Poleni wanafamilia wa mpendwa wetu poleni watanzania wenzangu. Tuendelee kushikamana katika kipindi hiki cha majonzi,” amesema Samatta, mchezaji wa zamani wa Aston Villa ya Uingereza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!