Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madiwani wakwapuaji waahidiwa kibano
Habari za Siasa

Madiwani wakwapuaji waahidiwa kibano

Spread the love

 

MAKAMU wa Rais Tanzania, Samia Suluhu Hassani amewaonya tabia ya madiwani kutumia fedha za mifuko ya kuwezesha wananchi kwa ajili ya masilahi yao binafsi ya kisiasa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tanga … (endelea).

Mama Samia metoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 17 Machi 2021, katika viwanja vya Tangamano, Tanga Mjini, ikiwa ni siku ya tatu kati ya tano ya ziara yake mkoani humo.

Amesema, diwani yeyote atakayebainika kutumia vibaya fedha hizo, atachukuliwa hatua.

“Wito wangu, mfuko huu sasa usitumike kama mfuko wa kisiasa kwa madiwani.”

“Ndugu zangu madiwani, mfuko huu mlikuwa mmeugeuza kujijenga kisiasa. kila mtu anavutia kwake, tumewafumbia macho kipindi hiki, kipindi kijacho nasimama na nyie,” amesema Mama Samia.

Ametoa onyo hilo baada ya kubaini upotevu wa fedha za mifuko ya uwezeshaji wananchi, ambapo inadaiwa baadhi ya madiwani wakati wa kampeni za uchaguzi huzitumia kuwapa wananchi ili kuwashawishi wawachague, kisha hazirudishwi.

“Kama mwaka huo umevuna Sh. 100 Mil zitakwenda kwa vikundi 50, kila kikundi mtapata 2 Mil. ukichukua hapo kila kikundi kuna watu watano, pesa hizo wanakwenda kugawana. Mikopo kwenye mifuko hairudishwi wanajua diwani wetu katupa, ukija uchaguzi mambo yake yameyea,” amesema Mama Samia.

Mama Samia ameshauri fedha hizo zigawiwe kwa vikundi vichache vitakavyoweza kuzifanyia kazi ili zirudishwe na kutolewa kwa wengine.

“Mifuko hii ni mimi na wewe, kuwepo tena itakuja kutokana na ufanisi wa mfuko huu, ni vyema kutoa kwa vikundi vichache vinavyotambulika wakafanya kazi wakarudisha pesa ikaenda katika vikundi vingine. Kuliko kila diwani apate haijulikani zimeenda wapi,” amesema Mama Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!