Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mambosasa aonya wanaomzushia Magufuli ugonjwa
Habari za Siasa

Mambosasa aonya wanaomzushia Magufuli ugonjwa

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

 

LAZARO Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, amewataka watu wanaosambaza taarifa, kwamba Rais John Magufuli mgonjwa, waache. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akijibu swali la waandishi wa habari leo Jumatano, tarehe 17 Machi 2021, jijini Dar es Salaam kuhusu watu wanaokamatwa kutokana na kile kilichodaiwa, kutoa taarifa za uzushi kwamba Rais Magufuli mgonjwa, amesema mtoa taarifa lazima ajiridhishe.

“Ninachosema kwa Watanzania, waache kuwa wazushi wa kupokea taarifa ambazo hawajazifuatilia wakijua ukweli wake, kuzisambaza na kuendelea kuvumisha uvumi ambao hauna maana,” amesema SACP Mambosasa.

Taarifa kwamba, kiongozi huyo ambaye hajaonekana hadharani kwa zaidi ya siku 17 sasa, zimekuwa zikitawala kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari ndani na nje.

Kamanda Mambosasa amewataka wananchi kuacha kusambaza taarifa hizo ambazo hazijathibitishwa ukweli wake.

Hadi sasa watu kadhaa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi katika maeneo mbalimbali kwa tuhuma za kusambaza taarifa hizo.

Jumatatu ya tarehe 15 Machi 2021, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassani aliwatoa hofu Watanzania akiwataka kupuuza taarifa hizo, kwa kuwa Rais Magufuli yu bukheri wa afya na anaendelea na majukumu yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!