Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mambosasa aonya wanaomzushia Magufuli ugonjwa
Habari za Siasa

Mambosasa aonya wanaomzushia Magufuli ugonjwa

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

 

LAZARO Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, amewataka watu wanaosambaza taarifa, kwamba Rais John Magufuli mgonjwa, waache. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akijibu swali la waandishi wa habari leo Jumatano, tarehe 17 Machi 2021, jijini Dar es Salaam kuhusu watu wanaokamatwa kutokana na kile kilichodaiwa, kutoa taarifa za uzushi kwamba Rais Magufuli mgonjwa, amesema mtoa taarifa lazima ajiridhishe.

“Ninachosema kwa Watanzania, waache kuwa wazushi wa kupokea taarifa ambazo hawajazifuatilia wakijua ukweli wake, kuzisambaza na kuendelea kuvumisha uvumi ambao hauna maana,” amesema SACP Mambosasa.

Taarifa kwamba, kiongozi huyo ambaye hajaonekana hadharani kwa zaidi ya siku 17 sasa, zimekuwa zikitawala kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari ndani na nje.

Kamanda Mambosasa amewataka wananchi kuacha kusambaza taarifa hizo ambazo hazijathibitishwa ukweli wake.

Hadi sasa watu kadhaa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi katika maeneo mbalimbali kwa tuhuma za kusambaza taarifa hizo.

Jumatatu ya tarehe 15 Machi 2021, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassani aliwatoa hofu Watanzania akiwataka kupuuza taarifa hizo, kwa kuwa Rais Magufuli yu bukheri wa afya na anaendelea na majukumu yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!