Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kesi ya Kambole kufutwa uwakili yapigwa kalenda
Habari MchanganyikoTangulizi

Kesi ya Kambole kufutwa uwakili yapigwa kalenda

Spread the love

 

KESI ya Wakili Jebra Kambole na mwenzake Edson Kilatu kufutiwa uwakili, iliyopangwa kusikilizwa leo Jumatatu tarehe 15 Machi 2021, katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imeaghirishwa hadi 19 Machi 2021. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kesi hiyo iliyofunguliwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), dhidi ya Wakili Kambole na Edson Kilatu, tarehe 8 Oktoba 2020, ilipangwa kusikilizwa na Kamati ya Maadili ya Mawakili leo Jumatatu katika mahakama hiyo, lakini akidi haikutimia.

Katika kesi hiyo, AG anamtuhumu Wakili Kambole na Wakili Kilatu kwamba walidharau mahakama pamoja na kukiuka maadili ya taaluma ya sheria.

Na kwamba AG, alipeleka mashtaka hayo kwenye Kamati ya Maadili ya Mawakili, akiiomba itamke kuwa mawakili hao wamekiuka maadili ya taaluma ya sheria, hivyo wafutiwe uwakili.

Katika kesi hiyo, Wakili Kambole anatuhumiwa kuidharau mahakama kwa kuchapisha maudhui katika ukurasa wake wa twitter kuwa ‘Kisutu Revenue Authority’ (Mamlaka ya Mapato Kisutu).

Mahakama Kuu ya Tanzania

Wakili Kambole anadaiwa kuchapisha maneno hayo baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwahukumu viongozi tisa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kulipa faini ya Sh. 350 milioni tarehe 10 Machi 2020.

Ni katika kesi namba 112 /2018, ambapo viongozi hao walikutwa na hatia ya makosa 12 ikiwemo kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali mwaka 2018.

Wakili Kilatu anatuhumiwa kuchapisha maoni kwenye ukurasa wake wa facebook tarehe 08 Agosti 2020, maoni ambayo yanadaiwa ni ya kuikosoa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, kutoiheshimu mahakama hiyo, sheria na taaluma ya sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!