Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kesi ya Kambole kufutwa uwakili yapigwa kalenda
Habari MchanganyikoTangulizi

Kesi ya Kambole kufutwa uwakili yapigwa kalenda

Spread the love

 

KESI ya Wakili Jebra Kambole na mwenzake Edson Kilatu kufutiwa uwakili, iliyopangwa kusikilizwa leo Jumatatu tarehe 15 Machi 2021, katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imeaghirishwa hadi 19 Machi 2021. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kesi hiyo iliyofunguliwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), dhidi ya Wakili Kambole na Edson Kilatu, tarehe 8 Oktoba 2020, ilipangwa kusikilizwa na Kamati ya Maadili ya Mawakili leo Jumatatu katika mahakama hiyo, lakini akidi haikutimia.

Katika kesi hiyo, AG anamtuhumu Wakili Kambole na Wakili Kilatu kwamba walidharau mahakama pamoja na kukiuka maadili ya taaluma ya sheria.

Na kwamba AG, alipeleka mashtaka hayo kwenye Kamati ya Maadili ya Mawakili, akiiomba itamke kuwa mawakili hao wamekiuka maadili ya taaluma ya sheria, hivyo wafutiwe uwakili.

Katika kesi hiyo, Wakili Kambole anatuhumiwa kuidharau mahakama kwa kuchapisha maudhui katika ukurasa wake wa twitter kuwa ‘Kisutu Revenue Authority’ (Mamlaka ya Mapato Kisutu).

Mahakama Kuu ya Tanzania

Wakili Kambole anadaiwa kuchapisha maneno hayo baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwahukumu viongozi tisa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kulipa faini ya Sh. 350 milioni tarehe 10 Machi 2020.

Ni katika kesi namba 112 /2018, ambapo viongozi hao walikutwa na hatia ya makosa 12 ikiwemo kufanya maandamano yasiyokuwa na kibali mwaka 2018.

Wakili Kilatu anatuhumiwa kuchapisha maoni kwenye ukurasa wake wa facebook tarehe 08 Agosti 2020, maoni ambayo yanadaiwa ni ya kuikosoa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, kutoiheshimu mahakama hiyo, sheria na taaluma ya sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!