Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Michezo Wachezaji watatu, timu ya Taifa Congo wakutwa na Corona
Michezo

Wachezaji watatu, timu ya Taifa Congo wakutwa na Corona

Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi wa michuano ya Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wandani (CHAN), wachezaji watatu wa timu ya Taifa ya Congo DR akiwemo mlinda mlango wao Nathan Mabruki wamekutwa na Corona na hivyo kuukosa mchezo wa leo dhidi ya Niger. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Wachezaji wengine ni William Luezi na Ricky Tulengi ambao wote kwa pamoja wamekutwa na maambukizi hayo mara baada ya kuchukuliwa vipimo saa chache kabla ya mchezo kama ilivyo kwenye kanuni za michuano hiyo.

Hii itakuwa mara ya pili kwa timu hiyo kukosa huduma ya baadhi ya nyota wake kutokana na kukutwa na virusi vya Corona, kama ilivyokuwa kwenye mchezo wa kwanza ambapo wachezaji wao watano walikaa nje kutokana na kukutwa na maambukizi hayo licha ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Bahati mbaya haikuishia hapo tu, kwenye mchezo wa pili wa kundi hilo dhidi ya Libya ambao walitoka sare ya bao 1-1, Congo DR walikosa huduma ya kocha wake, Florent Ibenge ambaye alikutwa na maambuki hayo.

Congo DR ambao ni vinara wa kundi B, baada ya kuwa na pointi nne, itacheza mchezo wake wa mwisho hii leo kwenye hatua hiyo dhidi ya Niger ambayo inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi mbili, huku kila timu ikiitaji ushindi wa aina yoyote kuweza kufuzu kwenye hatua inayofuata.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!