Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Stars kushuka dimbani, kuwakosa Nyoni, Bocco
Michezo

Stars kushuka dimbani, kuwakosa Nyoni, Bocco

John Bocco
Spread the love

 

TIMU ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inashuka dimbani kucheza na Namibia kwenye michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa pili kwa Taifa Stars, utachezwa Uwanja wa Limbe/Buea nchini Cameroon kunakofanyika mashindano hayo leo Jumamosi saa 4:00 usiku.

Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imesema, wachezaji watatu wa kikosi hicho kinachonolewa na Mburundi, Etienne Ndayiragijje ambao ni; John Bocco, Erasto Nyoni na Ibrahim Ame ambao wako chini ya uangalizi wa madaktari.

Erasto Nyoni

Wachezaji hao ambao wote kwa pamoja wanaitumikia Klabu ya Simba ya Dar es Salaam, waliukosa mchezo wa kwanza dhidi ya Zambia ambapo Stars ililala kwa magoli 2-0.

Stars iko kundi D pamoja na Zambia, Namibia na Guinea ambayo inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi tatu sawa na Zambia ambazo zote zilishinda michezo yao ya kwanza.

Mchezo wa leo Jumamosi, kati ya Stars na Namibia, zinakutana zikiwa na kumbukumbu ya kupoteza michezo yao ya kwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!