Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Stars kushuka dimbani, kuwakosa Nyoni, Bocco
Michezo

Stars kushuka dimbani, kuwakosa Nyoni, Bocco

John Bocco
Spread the love

 

TIMU ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inashuka dimbani kucheza na Namibia kwenye michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa pili kwa Taifa Stars, utachezwa Uwanja wa Limbe/Buea nchini Cameroon kunakofanyika mashindano hayo leo Jumamosi saa 4:00 usiku.

Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imesema, wachezaji watatu wa kikosi hicho kinachonolewa na Mburundi, Etienne Ndayiragijje ambao ni; John Bocco, Erasto Nyoni na Ibrahim Ame ambao wako chini ya uangalizi wa madaktari.

Erasto Nyoni

Wachezaji hao ambao wote kwa pamoja wanaitumikia Klabu ya Simba ya Dar es Salaam, waliukosa mchezo wa kwanza dhidi ya Zambia ambapo Stars ililala kwa magoli 2-0.

Stars iko kundi D pamoja na Zambia, Namibia na Guinea ambayo inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi tatu sawa na Zambia ambazo zote zilishinda michezo yao ya kwanza.

Mchezo wa leo Jumamosi, kati ya Stars na Namibia, zinakutana zikiwa na kumbukumbu ya kupoteza michezo yao ya kwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!