Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Michezo Stars kushuka dimbani, kuwakosa Nyoni, Bocco
Michezo

Stars kushuka dimbani, kuwakosa Nyoni, Bocco

John Bocco
Spread the love

 

TIMU ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inashuka dimbani kucheza na Namibia kwenye michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa pili kwa Taifa Stars, utachezwa Uwanja wa Limbe/Buea nchini Cameroon kunakofanyika mashindano hayo leo Jumamosi saa 4:00 usiku.

Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imesema, wachezaji watatu wa kikosi hicho kinachonolewa na Mburundi, Etienne Ndayiragijje ambao ni; John Bocco, Erasto Nyoni na Ibrahim Ame ambao wako chini ya uangalizi wa madaktari.

Erasto Nyoni

Wachezaji hao ambao wote kwa pamoja wanaitumikia Klabu ya Simba ya Dar es Salaam, waliukosa mchezo wa kwanza dhidi ya Zambia ambapo Stars ililala kwa magoli 2-0.

Stars iko kundi D pamoja na Zambia, Namibia na Guinea ambayo inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi tatu sawa na Zambia ambazo zote zilishinda michezo yao ya kwanza.

Mchezo wa leo Jumamosi, kati ya Stars na Namibia, zinakutana zikiwa na kumbukumbu ya kupoteza michezo yao ya kwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

TANROADS wawataka watumishi wazingatie michezo kazini

Spread the love  WAKALA wa barabara Tanzania (TANROADS) imesema michezo inapaswa kuzingatiwa...

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

error: Content is protected !!