Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Corona inavyoendelea kuitesa Afrika, dunia 
Habari Mchanganyiko

Corona inavyoendelea kuitesa Afrika, dunia 

Spread the love

MAAMBUKIZO ya virusi vya corona (COVID-19) duniani, yamefikia milioni 85.5, waliopona milioni 60.4 na waliopoteza maisha milioni 1.8. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hadi leo Jumatatu asubuhi tarehe 04 Januari 2021, Marekani inaongoza kwa maambukizo mengi duniani yaliyofikia milioni 21.1, waliofariki 360,078 na waliopona milioni 12.4.

India inashika nafasi ya pili ikiwa na maambukizo milioni 10.3, waliopona milioni 9.9 na waliofariki wakiwa 149,686.

Brazil ina maambukizo milioni 7.7 ikiwa nafasi ya tatu, waliofariki kutokana na ugonjwa huo wakiwa 196,018 na waliopona milioni 6.8.

Barani Afrika, Afrika Kusini, inaongoza kwa kuwa na maambukizo milioni 1.1, waliopona 903,679 na waliofariki wakiwa 29,577.

Morocco inashika nafasi ya pili Afrika ikiwa na maambukizo 443,146, waliopona 413,393 na vifo vikiwa 7,485.

Nchi za Afrika Mashariki, Kenya inaongoza kwa kuwa na maambukizo 96,802, waliopona 79,073 na vifo vikiwa 1685.

Kutokana na maambukizo hayo, baadhi ya mataifa, yamekuwa yakiweka mazuio ya kutosafiri au kutoka nje kwa kipindi Fulani ili kuzuia kusambaa zaidi kwa maambukizo hayo.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limekuwa likisisitiza kuchukuliwa kwa tahadhari ikiwemo kunawa mikono mara kwa mara na kuepuka mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!