Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mauaji mkesha wa Krismas
Habari za Siasa

Mauaji mkesha wa Krismas

Spread the love

WATU kadhaa wameuawa Kaskazini Mashariki mwa Nigeria baada ya wanamgambo wa Boko Haram kushambulia vijiji vya Wakristo na kuteketeza Kanisa wakati wa Mkesha wa Krismasi. inaripoti BBC…(endelea).

Vyanzo vya habari katika eneo hilo vinasema, karibu watu wa 11 wameuawa.

Wapiganaji waliingia Pemi katika Jimbo la Borno, kwa kutumia magari na piki piki na kuanza kufyatua risasi holela.

Pemi iko karibu na Chibok ambako wasichana 200 wa shule walitekwa mwaka 2014.

Boko Haram wamefanya mashambulio kadhaa Kaskazini mwa Nigeria ambako wanapigana kupindua serikali ili kubuni taifa la Kiislamu.

Wanavijiji walitorokea msituni na baadhi yao bado hawajulikani waliko.

“Magaidi waliwaua watu saba, kuchoma moto nyumba 10 na kuiba bidhaa za chakula ambazo zilikuwa zigawanyiwe wakaazi wakati wa sherehe ya Krismasi ,”kiongozi wa wanamgambo Abwaku Kabu alisema.

Wasambuliaji walichoma moto kanisa, kumteka mchungaji na kuiba bidhaa za matibabu katika hospitali moja kabla ya kuiteketeza moto.

Mzozo wa Boko Haram ambao umedumu kwa miongo kadhaa, umesababisha mauaji ya watu karibu 36,000 na wengine milioni mbili kufurushwa makwao, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!