Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli awatakia Watanzania Heri ya Krismas
Habari za Siasa

Rais Magufuli awatakia Watanzania Heri ya Krismas

Rais John Magufuli
Spread the love
RAIS wa Tanzania, Dk. John Magufuli ameungana na Watanzania kuadhimisha siku ya kuzaliwa Yesu Kristo, kwa kusali Misa Takatifu ya Krismasi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Misa hiyo imefanyika leo Ijumaa tarehe 25 Desemba 2020, katika Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Imakulata,  Chamwino mkoani Dodoma.

Kwa mujibu wa taarifa ya Gerson Msigwa, Mawasiliano ya Rais, misa hiyo iliongozwa na Paroko wa Parokia hiyo Padre Paul Mapalala.

“Rais Magufuli amewapongeza na kuwatakia heri Watanzania wote kwa sikukuu ya Krismasi na amewataka kuendelea kumshukuru Mungu kwa miujiza na upendo mkubwa anaolitendea Taifa la Tanzania,” inaeleza taarifa ya Msigwa.

Katika misa hiyo, Rais Magufuli amesema upendo na miujiza ya Mungu kwa Tanzania, inajidhihirisha katika kipindi hiki ambapo Dunia inapita katika wakati mgumu wa janga la ugonjwa wa Korona (Covid-19).

Ambapo maelfu ya watu wanaendelea kupoteza maisha kila siku, lakini Tanzania imeepushwa na janga hilo na maisha ya Watanzania yanaendelea kama kawaida.

Rais Magufuli ametoa wito kwa viongozi wa Mataifa mbalimbali duniani, kumweka Mungu mbele katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Korona, badala ya kutegemea nguvu za binadamu pekee.

1 Comment

  • Vatikani kuna Corona pamoja na Mecca na Madina na Israel
    Sasa wao wamekosea wapi? Hawakumuweka Mungu mbele?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!