Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo JPM: Simba, Yanga zimetuchelewesha
Michezo

JPM: Simba, Yanga zimetuchelewesha

Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli amesema wakati umefika kwa timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars) kuundwa bila ya kuwa na wahcezaji wanaotoka katika vikosi vya Simba na Yanga kwa kuwa klabu hizo mbili zimechelewesha katika kupiga hatua kwenye sekta hiyo ya michezo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Maneno hayo ameyasema jijini Dodoma wakati akitoa maagizo kwa waziri mpya wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa pamoja na Naibu waziri Abdalah Ulega mara baada ya zoezi la kuwaapisha.

Wakati akitoa maagizo hayo Rais Magufuli alisema kuwa haiwezekani kila tukienda kucheza tunashindwa, sasa inabidi tuwe na timu ya Taifa isiyokuwa na Simba na Yanga kwa kuwa zimetuchelesha.

“Tumekupeleka wizara ya michezo (Innocent Bashungwa) mkafanye kazi kweli, haiwezekani tunakwenda kucheza tunashindwa tu. Tunataka tukashinde na mambo ya kwenda na Simba na Yanga tu, imefika wakati tukawe na timu ya Taifa isiyokuwa na mahusiano ya Simba na Yanga,” alisema Rais Magufuli.

Rais John Magufuli

Kauli hiyo imekuja kufuatia kuwa asilimia kubwa ya wachezaji wanaoitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) wanatokea kwenye klabu za Simba na Yanga ambao wanatawala soka la Tanzania.

Kikosi kilichopita cha Taifa Stars ambacho kiliitwa na kocha Etiene Ndayilagije kilikuwa na jumla ya wachezaji 27 kati ya hao wachezaji waliotoka kwenye klabu za Simba na Yanga walikuwa 15.

Timu hiyo ambayo kwa sasa inawania kusaka tiketi ya kufuzu kwa michuano ya kombe la Mataifa Afrika inayotarajia kufanyika mwakani nchini Cameroon ambapo Taifa Stars ipo kundi J, sambamba na timu za Tunisia, Libya na Equatorial Guinea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!