Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa IGP Sirro awaita Lissu, Lema
Habari za SiasaTangulizi

IGP Sirro awaita Lissu, Lema

Spread the love

INSPEKTA Jenerali wa Polisi (IGP) nchini Tanzania, Simon Sirro amewataka wanasiasa waliokimbia nje ya nchi kwa madai ya kutishiwa usalama wa maisha yao kurejea nchini humo kwani kuna amani na yuko tayari kuwapa ulinzi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

IGP Sirro ametoa kauli hiyo leo Alhamisi tarehe 19 Novemba 2020 jijini Dar es Salaam,  wakati anazungumza na wanahabari kuhusu tathimi ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

Kauli hiyo ameitoa kipindi ambacho wanasiasa wawili wa upinzani, wameondoka Tanzania wakihofia usalama wa maisha yao.

Wanasiasa hao ni, Tundu Lissu, aliyekuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema aliyekwenda Ubelgiji na aliyekuwa mgombea Ubunge Arusha Mjini kupitia chama hicho, Godbless Lema aliyeko Kenya.

IGP Simon Sirro

“Nchi yetu ya amani na utulivu na kama wako nje warudi nchini kuna amani. Ni vizuri Watanzania wakaelewa kwamba, hili ni suala la mtu binafsi  anaamua kusema tu. Kimsingi tukipata taarifa hiyo niko tayari kumpa ulinzi na familia yake, ataishi kwa amani,” amesema IGP Sirro.

Akizungumzia sakata hilo, IGP amesema licha ya juhudi zake za kuiandika barua Chadema kumtaka Lissu na wanasiasa wengine wa chama hicho wanadai kutishiwa maisha kuripoti ofisini kwake, wanasiasa hao hawakutoa taarifa badala yake walikwenda kulalamika kwenye balozi za mataifa ya nje.

Godbless Lema

“Niliandika barua kwa Chadema aje aseme anatishiwa na nani maana unaweza kutishiwa na mtu mwingine hayo ni mambo ya kawaida unatishiwa unaenda kutoa taarifa ubalozi badala ya polisi,” amesema IGP Sirro.

IGP Sirro amesema “Lema kwenye uchaguzi tumezungumza sana, lakini yeye anatishiwa kuuawa hakuna taarifa iliyotolewa Polisi. Huo ni mkakati wa kutuchafua. Sisi jeshi hatuna habari yoyote ya kutishiwa kwa mtu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!