Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli atangazwa mshindi urais Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli atangazwa mshindi urais Tanzania

Rais John Magufuli
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemtangaza Dk. John Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Rais mteule wa Tanzania baada ya kupata kura milioni 12.5 kati ya milioni 15.9 zilizopigwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akitangaza matokeo hayo leo Ijumaa tarehe 30 Oktoba 2020, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage amesema, waliojiandilisha kupiga kura walikuwa milioni 29.

Amesema, waliopiga kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 walikuwa milioni 15.9.

Jaji Kaijage amesema, kura halali zilikuwa milioni 14.8. Mwenyekiti hiyo amesema, Tundu Lissu wa Chadema amepata kura milioni 1.9.

Tundu Lissu (katikati), Mgombea Urais Tanzania kwa tiketi ya Chadema

Jaji Kaijage amesema, Jumapili tarehe 1 Novemba 2020, itafanyika shughuli ya kukabidhi hati ya ushindi kwa Dk. Magufuli na mgombea wake mwenza, Samia Suluhu Hassan.

Katika uchaguzi mkuu uliomwingiza Magufuli madarakani mwaka 2015, Dk. Magufuli alipata kura milioni 8.88 sawa na asilimia 58.46 huku mshindani wake, Edward Lowassa wa Chadema alipata kura milioni 6.07 sawa na asilimia 39.97

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

error: Content is protected !!