Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli atangazwa mshindi urais Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli atangazwa mshindi urais Tanzania

Rais John Magufuli
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemtangaza Dk. John Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Rais mteule wa Tanzania baada ya kupata kura milioni 12.5 kati ya milioni 15.9 zilizopigwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akitangaza matokeo hayo leo Ijumaa tarehe 30 Oktoba 2020, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage amesema, waliojiandilisha kupiga kura walikuwa milioni 29.

Amesema, waliopiga kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 walikuwa milioni 15.9.

Jaji Kaijage amesema, kura halali zilikuwa milioni 14.8. Mwenyekiti hiyo amesema, Tundu Lissu wa Chadema amepata kura milioni 1.9.

Tundu Lissu (katikati), Mgombea Urais Tanzania kwa tiketi ya Chadema

Jaji Kaijage amesema, Jumapili tarehe 1 Novemba 2020, itafanyika shughuli ya kukabidhi hati ya ushindi kwa Dk. Magufuli na mgombea wake mwenza, Samia Suluhu Hassan.

Katika uchaguzi mkuu uliomwingiza Magufuli madarakani mwaka 2015, Dk. Magufuli alipata kura milioni 8.88 sawa na asilimia 58.46 huku mshindani wake, Edward Lowassa wa Chadema alipata kura milioni 6.07 sawa na asilimia 39.97

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!