Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli atangazwa mshindi urais Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli atangazwa mshindi urais Tanzania

Rais John Magufuli
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemtangaza Dk. John Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Rais mteule wa Tanzania baada ya kupata kura milioni 12.5 kati ya milioni 15.9 zilizopigwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akitangaza matokeo hayo leo Ijumaa tarehe 30 Oktoba 2020, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage amesema, waliojiandilisha kupiga kura walikuwa milioni 29.

Amesema, waliopiga kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 walikuwa milioni 15.9.

Jaji Kaijage amesema, kura halali zilikuwa milioni 14.8. Mwenyekiti hiyo amesema, Tundu Lissu wa Chadema amepata kura milioni 1.9.

Tundu Lissu (katikati), Mgombea Urais Tanzania kwa tiketi ya Chadema

Jaji Kaijage amesema, Jumapili tarehe 1 Novemba 2020, itafanyika shughuli ya kukabidhi hati ya ushindi kwa Dk. Magufuli na mgombea wake mwenza, Samia Suluhu Hassan.

Katika uchaguzi mkuu uliomwingiza Magufuli madarakani mwaka 2015, Dk. Magufuli alipata kura milioni 8.88 sawa na asilimia 58.46 huku mshindani wake, Edward Lowassa wa Chadema alipata kura milioni 6.07 sawa na asilimia 39.97

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia apangua mawaziri

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la...

Habari za Siasa

RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia

Spread the loveALIYEWAHI kuwa mkuu wa mikoa ya Dodoma, Mara, Mtwara na...

Habari za Siasa

Marekani kuwekeza Dola 500 Mil kupeleka bidhaa na huduma Tanzania

Spread the loveMAKAMU wa Rais wa Marekani, Kamala Harris amesema miongoni mwa...

Habari za Siasa

Kamala ataja hatua mpya kuimarisha uhusiano wa kibiashara Tanzania, Marekani

Spread the loveKATIKA kuimaridha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi baina ya Tanzania...

error: Content is protected !!