Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa IGP Sirro: Magaidi 300 walivamia Mtwara
Habari za Siasa

IGP Sirro: Magaidi 300 walivamia Mtwara

IGP Simon Sirro
Spread the love

INSPEKTA Jenerali wa Polisi (IGP) nchini Tanzania, Simon Sirro amesema, magaidi zaidi ya 300 kutoka Msumbiji walivamia Kijiji cha Kitaya Mkoa wa Mtwara na kufanya uhalifu mbalimbali ikiwemo mauji. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

“Madaigi wapatao 300 kutoka Msumbiji, walivamia Kijiji chetu cha Kitaya na kufanya uhalifu mbalimbali ikiwemo mauaji,” amesema IGP Sirro aliyekuwa anazungumzia hali ya usalama kuelekea Uchaguzi Mkuu tarehe 28 Oktoba 2020.

IGP Sirro amesema, “tumefuatilia baadhi ya watu, wamekamatwa na wengine ni wa kwetu hapa tumewakamata tunaendelea kuwahoji.”

“Ukifanya uhalifu Tanzania na damu ya Mtanzania haiwezi kwenda hivi, waliofanya mauaji wengine wamerudi Msumbiji na wengine tumewakamta.”

IGP Sirro amesema, “tunaendelea kupambana nao ili kuupata mtandao wote ulioanzia kule Kibiti na Rufiji ambao tulipambana nao wakaona wameshindwa.”

Mkuu huyo wa jeshi amesema, watahakikisha wanakamatwa iwe wanakwenda Msumbiji, Kenya au kwingineko ili “mwisho wa siku haki itandendeka na watakamatwa na kupelekwa mahakamani.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!