Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali ya Tanzania yawaonya viongozi wa dini
Habari za Siasa

Serikali ya Tanzania yawaonya viongozi wa dini

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania, amewaonya viongozi wote wa dini na jumuiya za kijamii kuepuka kutoa matamko ya kisiasa yenye lengo la kuhamisha na kuelekeza waumini wao kumchagua mgombea au chama fulani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Onyo hilo, limetoka ikiwa zimebaki siku takribani saba kabla ya Watanzania kupiga kura kuwachagua madiwani, wabunge na Rais katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatano tarehe 21 Oktoba 2020 na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania, George Simbachawene imesema, watakaoshindwa kutekeleza masharti, watachukuliwa hatua.

“Wiongozi watakaoshindwa kuzingatia masharti ya sheria za usajili wa jumuiya na katiba zao, wizara haitasita kuchukua hatua za kuifuta jumuiya hiyo au kutoisajili ambayo imewasilisha maombi yake,” amesema Waziri Simbachawene

Waziri huyo, amewataka viongozi hao, wazingatie sheria ya jumuiya ambayo inakataza viongozi wa kidini kujihusisha na vitendo hivyo, kwa kuwa “vinaingilia uhuru wa kikatiba wa kila mtu kumchagua mgombea anayemtaka.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!