Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi: Tunawashikilia maofisa watatu ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Polisi: Tunawashikilia maofisa watatu ACT-Wazalendo

Spread the love

POLISI Mkoa wa Kinondoni jijini Dar es Salaam nchini Tanzania, linawashikilia maofisa watatu wa chama cha upinzani cha ACT-Wazalendo katika kituo cha polisi Osterbay. Anaripoti Regina Mkonde, Kinondoni … (endelea).

Maofisa hao wanaoshikiliwa ni; Dotto Rangimoto (Afisa Habari Msaidizi), Dahlia Majid (Afisa wa Uchaguzi) na Arodia Peter (Afisa Habari na Uenezi) ambao inadaiwa walikamatwa na polisi Ijumaa iliyopita tarehe 25 Septemba 2020.

Maofisa hao walikamatwa wakiwa ofisi za chama hicho zilizopo Magomeni jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mussa Taibu akizungumza na MwanaHALISI Online leo Jumapili tarehe 27 Septemba 2020 amesema, hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kina kwa kuwa liko chini ya Idara ya Upelelezi Makao Makuu ya Jeshi la Polisi.

“Wapo katika Kito cha Oysterbay, lakini hawajakamatwa na Polisi Kinondoni, kwa hiyo siwezi kuzungumzia. Wako chini ya makao makuu ya upelelezi ndio maafisa wake wamewakamata,” amesema Kamanda Taibu.

Awali, MwanaHALISI Online ilimtafuta Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kupata ufafanuzi juu ya suala hilo, ambaye alijibu hana taarifa za kukamatwa kwa maafisa hao.

“Hizo taarifa ndio nazisikia kwako, sina taarifa za kwamba Jeshi la Polisi wamewakamata,” amesema Kamanda Mambosasa.

Janeth Rithe, Naibu Katibu wa Itikadi na Uenezi wa ACT-Wazalendo amesema, mawakili wa chama hicho wanafuatilia kama maafisa hao watapewa dhamana au watafikishwa mahakamani kesho Jumatatu tarehe 28 Septemba 2020.

“Toka jana wamekataa kuwatoa tulitafuta wanasheria kushughulikia, sababu leo sio siku ya kazi labda kesho watapelekwa mahakani tuon,” amesema Rithe.

MwanaHALISI Online linaendelea kutafuta uongozi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu kwa habari zaidi kuhusu suala hili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!