Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu atoa ahadi ‘mwiba’ kwa vigogo
Habari za SiasaTangulizi

Lissu atoa ahadi ‘mwiba’ kwa vigogo

Tundu Lissu, Mgombea Urais Tanzania kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameahidi kukwapua ardhi iliyotwaliwa na vigogo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Ifakara..(endelea).

Mbele ya wananchi wa Ifakara, Morogoro tarehe 12 Agosti 2020, kwenye kampeni za kusaka urais amesema, serikali atakayoiunda itawashughulikia wezi wa ardhi.

“Kama wamechukua ardhi kwa kiwango hiki, watakubalije mpinzani aingie na kuibua ufisadi wao?” Amehoji Lissu.

Amesema, atafanya mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa umiliki ardhi kwa kuwa, vigogo wengi wamekwapua ardhi ya wananchi.

“Kuna vigogo wengi wamejimilikisha ardhi hapa, wakubwa hawa wametumia madaraka yao vibaya, wameiba ardhi ya wananchi na kuwafanya wahangaike.

“Maelfu ya heka yamekaa bure kwasababu wakubwa wameyachukua. Wananchi wanahangaika, hawana pa kulima,”amesema Lissu.

Amewaambia wakazi wa Ifakara, kwamba endapo atapata ridhaa ya kuongoza, atakwapua mashamba hayo kutoka kwa vigogo wanaoyamiliki.

Amesema, baada ya kukwapua ardhi hiyo, ataikabidhi kwa wananchi waitumie kwa kilimo na ufugaji.

Amesema, Morogoro ni sehemu muhimu kwa uchumi wa nchi kwa kuwa, zaidi ya asilimia 70 ya sukari nchini inatoka kwenye ardhi ya mkoa huo.

“Bonde la Kilombero mpaka Mikumi linaweza kulisha nchi kwa mwaka mzima.

“Kuna matunda, samaki na hakuna zao linaloweza kukataa kustawi kwenye ardhi ya Morogoro, lakini mkoa huu umefanywa kama shamba la bibi,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

error: Content is protected !!