Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwakyembe aiambia CCM ‘kujaa mikutanoni si ushindi’
Habari za Siasa

Mwakyembe aiambia CCM ‘kujaa mikutanoni si ushindi’

Spread the love

HARRISON Mwakyembe, aliyekuwa mbunge wa Kyela kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ametahadharisha kwamba kujaa watu kwenye mikutano si hoja ya kushinda. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kyela…(endelea).

Akizungumza na wanachama wa chama hicho kwenye uzinduzi wa kampeni za jimbo hilo, jijini Mbeya amewataka wanachana hao kwenda kupiga kura tarehe 28 Oktoba 2020.

Amewataka wanachama hao kuacha kulumbana na badala yake, wasake kura za urais, mbunge na madiwani wa jimbo hilo.

Katika kura za maoni ndani ya CCM, Dk. Mwakyembe aliangushwa na Ally Mlaghila ambaye ndiye aliyepitishwa na chama hicho kugombea ubunge katika jimbo hilo.

“Ushindi haupatikani kwa wingi wa watu kujaa mikutano ya kampeni, bali kwa wingi wa kura,” amesema Dk. Mwakyembe.

Amesisitiza kuachana na dhana kwamba, ushindi tayari umepatikana kutokana na kutekelezwa kwa miradi mingi kwenye utawala wa Rais John Magufuli.

Hata hivyo, amewaomba wana Kyela kumpa kura Dk. Magufuli ambaye ni mgombea urais wa CCM, kutokana na juhudi zake za kuibadili Kyela na kuwa na taswira ya maendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

error: Content is protected !!