Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Raia saba wa kigeni mbaroni tuhuma uhalifu mtandaoni
Habari Mchanganyiko

Raia saba wa kigeni mbaroni tuhuma uhalifu mtandaoni

SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

RAIA saba wa kigeni wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam nchini Tanzania kwa tuhuma za uhalifu kwa njia ya mtandao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Watuhumiwa hao ni, Adewale Nuren Oyedes, raia wa Nigeria. Ibrahim Darbey (Liberia), Cream Milton Elias (Liberia), Basube Dominic (DRC), Prince Tito (Liberia), Sibongile Arthur (Afrika Kusini) na Baljit Singh (India).

Akizungumza na wanahabari leo Jumamosi tarehe 12 Septemba 2020 jijini Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polisi wa kanda hiyo amesema, watuhumiwa hao wamekamatwa nyakati tofauti, baada ya Polisi kufanya msako kati ya kipindi cha Agosti na Septemba 2020.

“Jeshi la Polisi katika maeneo mbalimbali ya Jiji, limefanya msako na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hawa ambao wamekuwa wakifanya utapeli na wizi kwa njia ya mtandao,” amesema Kamanda Mambosasa.

Kamanda huyo wa Polisi Dar es Salaam amesema, watuhumiwa hao baada ya kuhojiwa walikiri kujipatia fedha Sh.10 milioni kwa njia ya udanganyifu kupitia njia ya mtandao.

“Baada ya mahojiano walikiri kujipatia kiasi hicho cha fedha ambapo baadhi ya fedha hizo zilitumika kuanzisha duka la vinywaji vya pombe kali maeneo ya Tangi Bovu-Mbezi Beach, walinunua gari Toyota aina ya Mark X, televisheni mbili na magodoro,” amesema Kamanda Mambosasa.

Kamanda Mambosasa amesema, watuhumiwa hao saba watafikishwa mahakamani hivi karibuni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!