Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Milioni 4.9 zamkamatisha kigogo wa Takukuru
Habari Mchanganyiko

Milioni 4.9 zamkamatisha kigogo wa Takukuru

Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania, imemkamata ofisa wake wa uchunguzi mwandamizi, Nina Sipilon Saibul kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh.4.9 milioni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kinondoni … (endelea).

Taarifa iliyotolewa jana Ijumaa tarehe 11 Septemba 2020 na Doreen Kapwani, Ofisa Uhusiano wa Takukuru imesema, Nina alikamatwa jana Alhamisi.

Doreen alisema, Nina ambaye ni Afisa Uchunguzi ofisi ya Takukuru Kinondoni jijini Dar es Salaam, aliomba rushwa kutoka kwa mfanyabiashara mmoja wa Jiji hilo anayejishughulisha na shughuli za Real Estate.

“Takukuru Mkoa wa Kinondoni, ilipokea taarifa za malalamiko dhidi ya afisa wake, kuomba rushwa ili asiendelee na uchunguzi uliodaiwa ulikuwa ukiendelea ndani ya Takukuru dhidi ya mfanyabiashara huyo(mlalamikaji).”

“Baada ya taarifa hizo kupokelewa, uchunguzi wa awali wa kuthibitisha tuhuma hizo ulifanyika na kubaini upo ukweli wa madai ya kuomba hongo lakini hakukuwa na jalada wala uchunguzi wowote uliokuwa ukiendelea dhidi ya mlalamikaji,” amesema Doreen.

Alisema, Takukuru imechukua hatua hii ili kuhakikisha inajisafisha dhidi ya watumishi wake wachache wenye tabia ovu zenye kukichafua chombo hicho.

“Uchunguzi dhidi ya tuhuma hii unakamilishwa ili kuweza kuwafikisha watuhumiwa mahakamani mapema iwezekanavyo,” alisema Doreen.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!