Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wasafi FM yafungiwa siku 7
Habari Mchanganyiko

Wasafi FM yafungiwa siku 7

Spread the love

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetangaza kusitisha utoaji huduma za utangazaji kwa Wasafi FM kwa muda wa siku saba baada ya kukiuka kanuni za utangazaji kwa kutumia lugha za matusi kwenye kipindi cha The Switch na Mashamsham. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, James Kilaba akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa tarehe 11 Septemba 2020 jijini Dar es Salaam, amewataka Wasafi FM kutumia siku nzima ya leo kuomba radhi kutokana na ukiukwaji huo wa kanuni kwa kutumia lugha za matusi ambazo hazikubariki.

Kilaba amesema, adhabu hiyo itaanza kutumika kesho Jumamosi tarehe 12 hadi 18 Septemba 2020 na endapo Wasafi FM hawatatekeleza adhabu hiyo, TCRA itachukua hatua kali zaidi.

James Kilaba, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)

Mkurugenzi mkuu huyo, ametoa wito kwa Baraza la Habari Tanzania (MCT) kutumika kuonyana ili kunusuru adhabu hizo ambazo hawapendi kuzitoa.

Adhabu ambayo wameipata Wasafi FM inafanana na walioipta Clouds Televisheni na Clouds Redio ambazo TCRA iliifungia kwa siku saba kuanzia tarehe 28 Agosti hadi 3 Septemba 2020

Pia, TCRA ilitaka Clouds kutumia vituo vyake kuomba radhi tarehe 27 Agosti 2020 kutokana na ukiukwaji wa kanuni za utangazaji kupitia kipindi cha Clouds 360.

2 Comments

  • Wasafi si safi kama jina lao linavyojipambanua.
    Ukiangalia jinsi wanavyoimba nyimbo zao na matendo wanayoyaonyesha kwa jamii ni uchafu usiomithirika. Mara.nyingi hutumia maneno yenye ukakasi uliopitiliza. Bongo Flava inaharibu maadili ya vijana na watoto wa taifa hili. Wizara husika iko usingizini au bora license? Tujitafakari tusiige Kwa kisingizio cha usasa na utandawazi.
    Laiti ingekuwa enzi zile 1962 hadi 20215 wangeula wa chuya. Tuilinde tasnia ya mziki, utunzi na matendo mbele ya jamii.

  • Wako wapi magwiji wa mziki wa Bongo Flava au Mziki wa Kizazi Kipya?
    Uko wapi, Juma Nature na TMK, Afande Selle, Profesa Jay, Mr II Sugu, Ya Band Moto, Wagoso wa Kaya? Niliowataja walianzisha mziki wa kizazi kipya Kwa weredi wa kitukuka. Kazi Yao iliweza kupenya ktk vichwa vya jamii bula mikwaruzo. Hawakuiaibisha jamii kwani nyimbo zao ni nzuri kwa watoto na wazazi wao. Tujitafakari kwani tunaingia gizani tutapotelea huko!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!