Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Wasafi FM yafungiwa siku 7
Habari Mchanganyiko

Wasafi FM yafungiwa siku 7

Spread the love

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetangaza kusitisha utoaji huduma za utangazaji kwa Wasafi FM kwa muda wa siku saba baada ya kukiuka kanuni za utangazaji kwa kutumia lugha za matusi kwenye kipindi cha The Switch na Mashamsham. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, James Kilaba akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa tarehe 11 Septemba 2020 jijini Dar es Salaam, amewataka Wasafi FM kutumia siku nzima ya leo kuomba radhi kutokana na ukiukwaji huo wa kanuni kwa kutumia lugha za matusi ambazo hazikubariki.

Kilaba amesema, adhabu hiyo itaanza kutumika kesho Jumamosi tarehe 12 hadi 18 Septemba 2020 na endapo Wasafi FM hawatatekeleza adhabu hiyo, TCRA itachukua hatua kali zaidi.

James Kilaba, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)

Mkurugenzi mkuu huyo, ametoa wito kwa Baraza la Habari Tanzania (MCT) kutumika kuonyana ili kunusuru adhabu hizo ambazo hawapendi kuzitoa.

Adhabu ambayo wameipata Wasafi FM inafanana na walioipta Clouds Televisheni na Clouds Redio ambazo TCRA iliifungia kwa siku saba kuanzia tarehe 28 Agosti hadi 3 Septemba 2020

Pia, TCRA ilitaka Clouds kutumia vituo vyake kuomba radhi tarehe 27 Agosti 2020 kutokana na ukiukwaji wa kanuni za utangazaji kupitia kipindi cha Clouds 360.

2 Comments

  • Wasafi si safi kama jina lao linavyojipambanua.
    Ukiangalia jinsi wanavyoimba nyimbo zao na matendo wanayoyaonyesha kwa jamii ni uchafu usiomithirika. Mara.nyingi hutumia maneno yenye ukakasi uliopitiliza. Bongo Flava inaharibu maadili ya vijana na watoto wa taifa hili. Wizara husika iko usingizini au bora license? Tujitafakari tusiige Kwa kisingizio cha usasa na utandawazi.
    Laiti ingekuwa enzi zile 1962 hadi 20215 wangeula wa chuya. Tuilinde tasnia ya mziki, utunzi na matendo mbele ya jamii.

  • Wako wapi magwiji wa mziki wa Bongo Flava au Mziki wa Kizazi Kipya?
    Uko wapi, Juma Nature na TMK, Afande Selle, Profesa Jay, Mr II Sugu, Ya Band Moto, Wagoso wa Kaya? Niliowataja walianzisha mziki wa kizazi kipya Kwa weredi wa kitukuka. Kazi Yao iliweza kupenya ktk vichwa vya jamii bula mikwaruzo. Hawakuiaibisha jamii kwani nyimbo zao ni nzuri kwa watoto na wazazi wao. Tujitafakari kwani tunaingia gizani tutapotelea huko!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!