Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waliotafuna fedha za korosho matatani 
Habari za Siasa

Waliotafuna fedha za korosho matatani 

Spread the love

MAMA Samia Suluhu Hassan, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) iwashughulikie watu waliodhurumu fedha za malipo ya korosho kupitia Chama cha Ushirika cha Msingi cha Mazao(AMCOS). Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara … (endelea).

Samia ametoa agizo hilo leo Alhamisi tarehe 10 Septemba 2020 wakati akihutubia mkutano wa kampeni za CCM katika Uwanja wa Polisi Jimbo la Nanyamba mkoani Nanyamba mkoani Mtwara.

Samia ameiagiza Takukuru ihakikishe waliodhurumiwa fedha za korosho walipwe stahiki zao.

“Kulikuwa na deni kubwa la korosho na Serikali tumelipa lote, lakini viongozi wa AMCOS wameangalia nani hajui kusoma pesa zao wakazichukua, naiagiza Serikali ya Mkoa kila aliyedhurumiwa kupitia Takukuru pesa ipatikane,” amesema Samia.

Amesema Serikali inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli imelipa deni lote la fedha za korosho, hivyo wanaolalamika hawajapata fedha mamlaka husika zinatakiwa zitafute ufumbuzi wa mahali ziliko fedha zao.

“Serikali tumelipa deni lote, lakini viongozi wa ushirika wanafanya mambo yasiyoingilika akilini, Rais Magufuli alishatoa Sh.20 bilioni kwa malipo ya Korosho, zipo Mtwara zitafutwe wapi zimeingia wanaodai walipwe pesa zao,” amesema Samia.

Mgombea huyo wa urais amemaliza mkutano wake wa kwanza kati ya miwili na sasa ameondoka kwenda kuendelea na mkutano mwingine mkoani humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!