WAGONJWA milioni 20.1 waliokuwa wameambukizwa virusi vya corona (COVID-19) duniani wamepona. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Mtandao wa worldometer umeripoti leo Alhamisi tarehe 10 Septemba 2020 kuwa, maambikizo duniani yamefikia milioni 28.04 huku waliopoteza maisha kutokana na ugonjwa huo ni 908,434.
Marekani imeendelea kuwa taifa linaloongoza dunia kwa kuwa na maambukizo milioni 6.5 ambapo waliopona ni milioni 3.8 na waliopoteza maisha ni 195,245.
China ambako corona ilianzia, ina maambukizo 85,153 kati yao, waliopoteza maisha ni 4,634 na waliopona ni 80,358.
Leave a comment