Friday , 17 May 2024
Home Kitengo Michezo Wawa, Miquison warejea kikosini, Kuwavaa Namungo Jumapili
Michezo

Wawa, Miquison warejea kikosini, Kuwavaa Namungo Jumapili

Spread the love

WACHEZAJI wa klabu ya Simba, Pascal Wawa na Luis Miquison wamerejea leo kikosini kwa kuingia kambini baada ya kuwasili leo nchini kutoka kwenye nchi zao walipokuwa wameenda kimapumziko. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Wachechaji hao ambao wamerudi nchini leo mchana na watakuwa sehemu ya kikosi kitakachosafiri kwenda Jijini Arusha ambapo Simba itakuwa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Namungo FC, utakaochezwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Wachezaji hao waliondoka nchini mara baada ya msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2019/20 kumalizika na wote kwa nyakati tofauti walienda kufunga ndoa.

Miquison alifunga ndoa yake na mwenza wake tarehe 22 Agosti, 2020 kama taarifa kutoka kwenye uongozi wa klabu hiyo zilivyoeleza.

Taarifa za kurejea kwao zimetolewa kupitia kurasa za mitandao ya kijamii ya klabu hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Uingereza, Hispania, Italia na Ufaransa kinawaka leo

Spread the loveLIGI mbalimbali barani ulaya kuendelea leo na michezokadhaa mikali itakwenda...

Michezo

Leo mkwanja upo Meridianbet, usipishane nao

Spread the love  Siku ya leo ni nzuri sana kwa wewe mtumiaji...

Michezo

Anza wikendi yako na Meridianbet, upige mkwanja wa maana

Spread the love Siku ya leo ni nzuri sana kwa wewe mtumiaji...

Habari MchanganyikoMichezo

Arafat atoka bima na kurejea kwenye benki

Spread the loveRais wa Zanzibar Hussein Mwinyi amemteua Arafat Ally Haji kuwa...

error: Content is protected !!