Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Sakata la THRDC: LHRC yaiangukia serikali ya Tanzania
Habari Mchanganyiko

Sakata la THRDC: LHRC yaiangukia serikali ya Tanzania

Flugence Massawe, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania (LHRC)
Spread the love

FLUGENCE Massawe, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania (LHRC), ameshauri mamlaka husika (Wizara ya Mambo ya Ndani) kutatua utata ulioibuka dhidi ya Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

“LHRC tunaamini kwamba, mamlaka husika zitalishughulikia suala hili kwa haraka, ili kuiwezesha taasisi ya THRDC kuendelea na kazi zake,” inaeleza taarifa iliyotolewa na Massawe kwa vyombo vya habari leo tarehe 19 Agosti 2020.

Aidha, LHRC imeeleza kuwa, imeshtushwa na taarifa za THRDC kusitisha shughuli zake huku ikitoa pole kwa uongozi wa mtandao huo kufuatia changamoto inazopitia wakati huu.

           Soma zaidi:-

“LHRC tumeshtushwa sana na taarifa zilizotolewa na THRDC kuhusu kusitisha shughuli zake kwa muda kufuatia kufungwa kwa akaunti za benki za taasisi hiyo.”

“Tunatoa pole kwa Bodi ya Wakuruenzi mratibu na wanachama kwa usumbufu wanaoupitia,” imeeleza taarifa ya LHRC.

THRDC uliitangazia umma wa Tanzania tarehe 17 Agosti 2020 kwamba unasitisha shughuli zake, baada ya kukumbwa na changamoto za kifedha za uendeshaji, kufuatia akaunti yake katika Benki ya CRDB kufungwa na Jeshi la Polisi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Vicky Ntetema, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya THRDC , Jeshi la Polisi limefunga akaunti hiyo, ili kufanyia kazi masuala yaliyoko mbele yake.

Hata hivyo, taarifa hiyo inaeleza kwamba, Onesmo Ole Ngurumwa, Mratibu wa THRDC siku ya Jumatatu alihojiwa na Jeshi la Polisi kuhusu tuhuma zinazo kabili mtandao huo, za kutowasilisha mikataba yake na wafadhili katika Ofisi ya Hazina na Ofisi ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!