Tuesday , 14 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aifariji familia ya Mkapa
Habari za Siasa

Rais Magufuli aifariji familia ya Mkapa

Rais John Magufuli akimpa pole Mama Anna Mkapa. Pembeni Mama Janeth Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amefika nyumbani kwa Hayati Rais wa awamu ya tatu wa nchi hiyo, Benjamini William Mkapa, Masaki jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Magufuli akiwa ameambatana na mkewe, Janeth wametoa mkono wa pole kwa Anna, mjane wa Mkapa, ndugu, jamaa na marafiki waliopo msibani hapo.

Mara baada ya kuwasilia, Rais Magufuli na Janeth walikwenda moja kwa moja eneo maalum lililoandaliwa kwa ajili ya kusaini kitabu cha maombolezo.

Wawilia hao baada ya kuamliza, walikwenda ndani kuwasafiri wafiwa akiwemo Anna.

Mkapa alifariki dunia usiku wa kuamkia jana Ijumaa tarehe 24 Julai 2020 katika moja ya hospitali jijini Dar es Salaam.

Mwili wa Mkapa utaagwa kwa siku tatu katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam kuanzia kesho Jumapili hadi Jumanne tarehe 28 Julai 2020 kisha utasafirishwa kwenda kijijini kwake, Lupaso Mkoa wa Mtwara kwa maziko yatakayofanyika Jumatano tarehe 29 Julai 2020.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Bunge kumuweka katibu mkuu wa EAC kikaangoni

Spread the loveAliyekuwa Katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dk. Peter...

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wizara kutumia Sh. 3.5 bilioni kuchunguza afya ya akili, nguvu za kiume

Spread the loveWIZARA ya Afya, imepanga kutumia Sh. 3.50 bilioni, kwa ajili...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC yapaza sauti changamoto ya intaneti

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umeitaka...

error: Content is protected !!