Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aifariji familia ya Mkapa
Habari za Siasa

Rais Magufuli aifariji familia ya Mkapa

Rais John Magufuli akimpa pole Mama Anna Mkapa. Pembeni Mama Janeth Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amefika nyumbani kwa Hayati Rais wa awamu ya tatu wa nchi hiyo, Benjamini William Mkapa, Masaki jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Magufuli akiwa ameambatana na mkewe, Janeth wametoa mkono wa pole kwa Anna, mjane wa Mkapa, ndugu, jamaa na marafiki waliopo msibani hapo.

Mara baada ya kuwasilia, Rais Magufuli na Janeth walikwenda moja kwa moja eneo maalum lililoandaliwa kwa ajili ya kusaini kitabu cha maombolezo.

Wawilia hao baada ya kuamliza, walikwenda ndani kuwasafiri wafiwa akiwemo Anna.

Mkapa alifariki dunia usiku wa kuamkia jana Ijumaa tarehe 24 Julai 2020 katika moja ya hospitali jijini Dar es Salaam.

Mwili wa Mkapa utaagwa kwa siku tatu katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam kuanzia kesho Jumapili hadi Jumanne tarehe 28 Julai 2020 kisha utasafirishwa kwenda kijijini kwake, Lupaso Mkoa wa Mtwara kwa maziko yatakayofanyika Jumatano tarehe 29 Julai 2020.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!