Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli: Balozi Lusinde alikuwa mzalendo wa kweli
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli: Balozi Lusinde alikuwa mzalendo wa kweli

Rais John Magufuli akisaini kitabu cha maombelezo ya kifo cha Balozi Job Lusinde
Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Maguful ametoa pole kwa familia ya Balozi Mstaafu Job Lusinde aliyefariki dunia tarehe 07 Julai, 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema, Rais Magufuli amekwenda msibani kwa Balozi Lusinde nyumbani kwake Kilimani Jijini Dodoma leo Alhamisi tarehe 9 Julai 2020.

Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amekwenda nyumbani hapo akitokea Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete Jijini Dodoma ambako ameongoza Kikao cha Kamati ya Maadili na Usalama na Kikao cha Kamati Kuu ya CCM.

Akiwa nyumbani kwa Marehemu Balozi Mstaafu Lusinde, Rais Magufuli amekutana na Mjane wa Marehemu, Sara Lusinde, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu ambapo ameeleza kuguswa na kifo cha Balozi Mstaafu Lusinde.

Amesema, daima atamkumbuka kwa mchango wake alioutoa akiwa waziri wa ujenzi, ushauri wake mzuri na moyo wake wa upendo na ukweli.

Rais John Magufuli akiwapa pole wafiwa, nyumbani kwa Marehemu Balozi Job Lusinde

Rais Magufuli ameeleza wakati wa utumishi wake, Balozi Mstaafu Lusinde alikuwa mzalendo wa kweli, mchapakazi na aliyetetea maslahi ya Tanzania na kwamba hata alipostaafu aliisemea vizuri Dodoma.

Amewataka wafiwa wote kuwa wastahimilivu na kumpuzisha salama hapo kesho Ijumaa tarehe 10 Julai, 2020 atakapozikwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa aanika mafanikio ya TMA

Spread the loveSHUGHULI za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), zimeimarika...

error: Content is protected !!