Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli ampongeza Rais mpya wa Malawi
Habari za Siasa

Magufuli ampongeza Rais mpya wa Malawi

Lazarus Chakwera, Rais wa Malawi
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amempongeza Dk. Lazarus Chakwera kuwa Rais mpya wa Malawi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Chakwera amechaguliwa na Wamalawi katika uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 23 Juni 2020 kwa kupata asilimia 58 akimshinda Rais aliyekuwa madarakani Peter Mutharika.

Uchaguzi huo ulifanyika baada ya ule wa awali wa Mei 2019 kufutwa na mahakama Februari 2020 baada ya kubaini ulikuwa na dosari.

Soma zaidi:-

Dk. Chakwera aliwasilisha maombi hayo mahakamani yaliyompa ushindi na katika uchaguzi wa marudio, aliwakilisha vyama zaidi ya vitano vya upinzani vilivyomng’oa Mutharika.

Tarehe 28 Juni 2020, Dk. Chakwera aliapishwa kuwa Rais wa Malawi.

Leo Jumatano tarehe 1 Julai 2020, Rais Magufuli ametumiw akaunti yake ya kijamii ya Twitter kumpingeza Rais Chakwera.

Rais Magufuli amesema, “Nakupongeza Dkt. Lazarus Chakwera kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Malawi.”

“Kwa niaba ya Serikali na Watanzania wote, naahidi kuendeleza uhusiano wetu wa kidugu, kirafiki na ujirani mwema hususani katika masuala ya uchumi na ustawi wa jamii. Hongera sana Mhe. Rais,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!