Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Sh. 170,000 yamponza Hakimu, mzazi mwenzake kufikishwa kortini
Habari Mchanganyiko

Sh. 170,000 yamponza Hakimu, mzazi mwenzake kufikishwa kortini

Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), itamfikisha mahakamani Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kilimatinde, Manyoni, Bahati Ilikunda na mzazi mwenzake, Haji Bwegege wanaotuhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya Sh. 350,000. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida…(endelea).

Taarifa ya Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Singida, Adili Elinipenda leo Jumatatu tarehe 29 Juni 2020 amesema, ofisi yake ilipokea kutoka kwa mwananchi mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa kuwa Bahati anaomba rushwa ya Sh. 350,000.

Amesema, ilia toe upendeleo kwa mtoa taarifa kwenye shauri la madai namba 03/2020, shauri ambalo lipo mbele yake.

Elinipenda amesema, tarehe 28 Juni 2020 wilayani Manyoni Mkoa wa Singida maeneo ya kituo cha mabasi yanaendayo Dodoma, ofisi hii ilimkatama Haji Juma Bwegege ambaye ni mzazi mwenzake na Baki baada ya kupokea rushwa ya Sh. 170,000 ikiwa ni sehemu ya Sh.350,000.

“Uchunguzi wa Takukuru Mkoa wa Singida umejiridhisha Haji Bwegege na Bahati Ilikunda wana mahusiano ya kifamilia (wana motto waliyezaa pamoja) jambo linaloashiria uwezekano wa Bahati kumtumia Haji katika kupokea rushwa anazoziomba,” amesema Elinipenda.

          Soma zaidi:-

Amesema, ofisi ya Takukuru inatoa shukuran za dhati kwa Idara ya Mahakama mkoani humo kwa jinsi wanavyoshirikiana kwenye mapambano dhidi ya rushwa kuanzia Mahakama ya Mwanzo hadi Mahakama ya Mkoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!