Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mufti Zubeir: Hakuna hijja
Habari Mchanganyiko

Mufti Zubeir: Hakuna hijja

Aboubakar Zubeir, Mufti wa Tanzania
Spread the love

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), limesema mwaka huu hakutakuwa na ibada ya Hijja, kutokana na janga la Virusi vya Corona. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Alhamisi tarehe 25 Juni 2020 na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir Ally wakati anazungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Mufti Zubeir amesema, hatua hiyo imetokana na zuio lililotolewa na nchi ya Saudi Arabia, kwa waumini wa Dini ya Kiislamu kutoka nje ya nchi hiyo, kufanya ibada hiyo, ili kudhibiti maambukizi ya Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu, inayosababishwa na Virusi vya corona (Covid-19).

Sambamba na hilo, Mufti Zubeir ameagiza madrasa zote nchini kufungulia kuanzia leo, huku akiwataka viongozi wa madrasa hizo, kufuata taratibu zote za kiafya, kwa ajili ya kujikinga na Covid-19.

Agizo hilo la kufunguliwa kwa madrasa, limekuja baada ya Rais John Magufuli, kuagiza shule zote nchini, kufunguliwa kuanzia Jumatatu ya tarehe 29 Juni 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

error: Content is protected !!