Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Masauni kada wa 17 kuchukua fomu CCM Z’bar
Habari za Siasa

Waziri Masauni kada wa 17 kuchukua fomu CCM Z’bar

Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania akichukua fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM
Spread the love

HAMAD Masauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi leo tarehe 22 Juni 2020, amejitokeza kuchukua fomu kuomba kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) visiwani Zanzibar kugombea urais. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Kada huyo na waziri alijitokeza katika ofisi kuu za CCM zilizopo Kisiwandui mjini Zanzibar.

Masauni anafanya idadi ya makada wa chama hicho waliojitokeza kuomba kuteuliwa visiwani humo kufika 17. Miongoni mwa waliojitokeza mpaka sasa ni Shamsi Vuai Nahodha, Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar; Hussein Ali Mwinyi, Waziri wa Ulinzi.

Wengine ni Balozi Ali Karume, mtoto wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar marehemu Sheikh Abeid Aman Karume: Jecha Salim Jecha, aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Mbwana Bakari Juma, Mbwana Yahya Mwinyi na Omar Sheha Mussa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!