Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hawa nusura niwatumbue leo – Rais Magufuli
Habari za Siasa

Hawa nusura niwatumbue leo – Rais Magufuli

Jonathan Shana, Kamanda wa Polisi Arusha
Spread the love

RAIS John Magufuli amesema, Jonathan Shana ambaye ni Kamanda wa Polisi Arusha na Frida Wikesi, Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani humo, ilikuwa awatimue kazi leo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

“Kamanda wa Polisi Arusha na Mkuu wa Takukuru Arusha nilikuwa niwatoe leo, ila nimewasamehe, Sijawasamehe moja kwa moja, najua salamu zitafika. Waambie wakafanye kazi nilizowatuma. Wasimamie sheria sio wafanye kazi zao,” amesema.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 22 Juni 2020, wakati akiwaapisha viongozi wapya – Iddi Kimanta (Mkuu wa Mkoa wa Arusha), Kena Kihongosi (Mkuu wa Wilaya ya Arusha) na Dk. John Pima (Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha), Ikulu jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo amesema, ameamua kuwasamehe kwa sharti la kutorudia tena makosa yao, na kwamba hatosita kuwafuta kazi kama hawatabadilisha mienendo yao.

“Na leo ilikuwa niwatoe RPC pamoja na mkuu wa TAKUKURU Arusha lakini nimeona niwaonye hapahapa, nimeamua kuwasamehe lakini sio moja kwa moja, wakifanya kosa lolote wataondoka. Nataka wakafanye kazi nilizowatuma sio wanazojituma wao,” amesema Rais Magufuli.

Frida Wikesi, Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Arusha

Kiongozi huyo wa nchi amemtuma Iddi kuwafikishia salamu Kamanda Shana na Wikesi, kwamba wanatakiwa kufanya kazi alizowatuma na si kufanya kazi wanazojituma wenyewe.

“Najua mtawafikishia salamu, nimejitahidi sana kuwasamehe, haiwezekani mmetwauma kazi za serikali wanafanya za kwao, RC Arusha kawafikishie ujumbe wafanye kazi walizotumwa kulingana na mamlaka yao, wasimamie sheria na maadili yao,” amesema Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli amewataka watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!