Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge upinzani akimbilia CCM
Habari za Siasa

Mbunge upinzani akimbilia CCM

Spread the love

REHEMA Migira, Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Wananchi (CUF), amekimbilia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora…(endelea).

Akitangaza kwenye sherehe ndogo iliyofanywa na chama hicho Tabora leo tarehe 15 Juni 2020, Rehema amesema, amejiunga na chama hicho baada ya kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais John Magufuli ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Taifa.

“Nikiwa na akili zangu timamu na kwa utashi wangu mimi mwenyewe, nimeamua kwa ridhaa yangu mimi mwenyewe bila kushikiwa mtutu wa bunduki kurudi chama cha mapinduzi,” amesema huku akipigiwa vigelegele na kuongeza:

“…maamuzi haya sikuyafanya eti kwa sababu napenda rangi za kijani, kuna sababu ambazo zimepelekea mimi leo niamue kurudi chama cha mapinduzi, CCM imekuwa ni ya wazalendo.”

Amesema, sera za CCM zinatekelezwa kupitia Rais Magufuli kwa kushirikiana na wasaidizi wake. “Vitendo hivyo vimesababisa hata sisi wapinzani tushawishike,” amesema.

1 Comment

  • Mtoa post rekebisha lugha, hakuna anae hamia ccm, bali wanarudi ccm, maana walitoka humo humo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!