Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge upinzani akimbilia CCM
Habari za Siasa

Mbunge upinzani akimbilia CCM

Spread the love

REHEMA Migira, Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Wananchi (CUF), amekimbilia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora…(endelea).

Akitangaza kwenye sherehe ndogo iliyofanywa na chama hicho Tabora leo tarehe 15 Juni 2020, Rehema amesema, amejiunga na chama hicho baada ya kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais John Magufuli ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Taifa.

“Nikiwa na akili zangu timamu na kwa utashi wangu mimi mwenyewe, nimeamua kwa ridhaa yangu mimi mwenyewe bila kushikiwa mtutu wa bunduki kurudi chama cha mapinduzi,” amesema huku akipigiwa vigelegele na kuongeza:

“…maamuzi haya sikuyafanya eti kwa sababu napenda rangi za kijani, kuna sababu ambazo zimepelekea mimi leo niamue kurudi chama cha mapinduzi, CCM imekuwa ni ya wazalendo.”

Amesema, sera za CCM zinatekelezwa kupitia Rais Magufuli kwa kushirikiana na wasaidizi wake. “Vitendo hivyo vimesababisa hata sisi wapinzani tushawishike,” amesema.

1 Comment

  • Mtoa post rekebisha lugha, hakuna anae hamia ccm, bali wanarudi ccm, maana walitoka humo humo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!