Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Corona yatikisa Kenya, watumishi wanne Ikulu waambukizwa
Kimataifa

Corona yatikisa Kenya, watumishi wanne Ikulu waambukizwa

Msemaji wa Ikulu ya Kenya, Kanze Dena
Spread the love

UGONJWA unaosababishwa na virusi vya corona (COVID-19) umeendelea kutikisa nchini Kenya, baada ya watumishi wanne wa Ikulu kubainika kuwa na ugonjwa huo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea)

Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu tarehe 15 Juni 2020 na Msemaji wa Ikulu ya Kenya, Kanze Dena imesema, watumishi hao wamebainika kuwa na corona baada ya watumishi wote wa Ikulu kupimwa.

Dena amesema, watumishi hao wamepelekwa hospitalini kwa matibabu zaidi na uangalizi.

“Uchunguzi ulifanyika kwa watumishi wote akiwemo Rais (Uhuru Kenyatta) na familia yake,” amesema Dena.

Katika taarifa yake, Dena amesema, Rais Kenyatta na familia yake wako salama, hawana maambukizo ya COVID-19.

Taarifa hiyo ya Dena imetolewa muda mfupi baada ya ile ya Katibu wa Baraza la Mawaziri la Afya wa Kenya, Mutahi Kagwe inayoonyesha wagonjwa wapua 133 wamebainika ndani ya saa 24 zilizopita.

Kenya imekuwa na utaratibu wa kutoa taarifa za maambukizo ya COVID-19 kila siku.

Amesema, wagonjwa wa corona wamefikia 3,727.

Kangwe amesema, wagonjwa waliopona wamefikia 1,286 baada ya wagonjwa 33 kuruhusiwa kutoka hospitalini ndani ya saa 24 zilizopita huku mgonjwa mmoja akipoteza maisha hivyo kufikisha idadi ya waliofariki kwa ugonjwa huo wakiwa 104.

Hali ya maambukizo duniani ya COVID-19 kwa mujibu wa mtandao wa worldometer yanaonyesha yamefikia milioni 8.02, waliopona ugonjwa huo wakiwa milioni 4.04 na waliopoteza maisha wakiwa 436,218.

Taifa la Marekani limeendelea kuongoza duniani kwa kuwa na wagonjwa wengi, milioni 2.16, waliopoteza maisha 117,859 huku waliopona wakiwa 870,077.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Faye amteua aliyekuwa mfungwa mwenzie kuwa waziri mkuu

Spread the loveRais mpya wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, amemteua Ousmane Sonko...

error: Content is protected !!