Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama: Mdee ana kesi ya kujibu, mashahidi watano kumtetea
Habari za Siasa

Mahakama: Mdee ana kesi ya kujibu, mashahidi watano kumtetea

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe akiwa mahakamani Kisutu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, imesema Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee  anayekabiliwa na kesi ya uchochezi kwa kutoa maneno ya kuudhi dhidi ya Rais John Magufuli ana kesi ya kujibu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Uamuzi huo umetolewa leo Alhamisi tarehe 28 Mei 2020 na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Hakimu Simba amesema, mahakama hiyo imemkuta  Mdee na kesi ya kujibu na kwamba anatakiwa kuwasilisha utetezi wake mahakamani hapo

Uamuzi huo  umetokana na upande wa mashtaka kufunga pazia la ushahidi wake tarehe 20 Februari 2020.

Mdee kupitia wakili wake, Hekima Mwasipo amedai mteja wake atajitetea kwa kiapo na atakuwa na mashahidi watano.

Inadaiwa tarehe 3, Julai 2017, katika Makao Makuu ya Ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) iliyopo mtaa wa Ufipa wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, Mdee anadaiwa kutamka maneno dhidi ya  Rais John Magufuli kuwa, “anaongea hovyohovyo, anatakiwa  afungwe breki”  na kwamba kitendo ambacho kingeweza  kusababisha uvunjifu wa amani.

Mdee alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza tarehe 10 Julai  2017, na kushtakiwa kwa mashtaka ya uchochezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!