Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Ndugulile azungumzia kutumbuliwa kwake
Habari za Siasa

Dk. Ndugulile azungumzia kutumbuliwa kwake

Dk. Faustine Ndugulile, aliyekuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Afya
Spread the love

DK. Faustine Ndugulile, amemshukuru Rais wa Tanzania, John Pombe Mangufuli kumteua kufanya kazi kama naibu waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Shukrani hizo za Dk. Ndugulile amezitoa leo Jumapili tarehe 17 Mei, 2020 kupitia akaunti yake ya Twitter ikiwa ni saa chache kupita tangu uteuzi wake ulipotenguliwa.

Jana Jumamosi, saa 2 usiku wa tarehe 16 Mei, 2020, Rais Magufuli alitangaza kumteua Dk. Godwin Mollel ambaye pia ni mbunge wa Siha (CCM) kuwa naibu waziri wa afya huku uteuzi wa Dk. Ndugulile ukitenguliwa.

Dk. Ndugulile ambaye ni mbunge wa Kigamboni kupitia CCM jijini Dar es Salaam, alihudumu katika nafasi ya naibu waziri kuanzia tarehe 9 Oktoba, 2017 akichukua nafasi ya Dk. Hamisi Kigwangalla aliyeteuliwa kuwa waziri wa maliasili na utalii.

“Nimepokea uamuzi wa Mhe Rais kwa unyenyekevu mkubwa. Ninamshukuru sana JPM kwa kunipa fursa ya kuhudumu katika Serikali yake.”

“Nawashukuru sana @umwalimu na watendaji wote kwa ushirikiano walionipatia. Mafanikio ya sekta ni makubwa sana. Namtakia kila la kheri NW ajaye Dkt Mollel.,” ameandika Dk. Ndugulile.

Malcolm @shilinde_cc amechangia ujumbe huo wa Dk. Ndugulile akisema,”Utumishi wako uliotukuka umeonekana, Watanzania wameona, you can be proud of that.,”

Naye fredy @fredy08122355 amesema,”Endelea kuwatumikia wapiga Kura wako, kazi uliyopewa, uliifanya kwa weledi mkubwa, hongera Sana Dr! ulikuwa miongoni mwa viongozi wanyenyekevu sana.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!