Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama Mtwara yamwachia huru Mwambe
Habari za Siasa

Mahakama Mtwara yamwachia huru Mwambe

Spread the love

MAHAKAMA ya Mkoa wa Mtwara leo tarehe 30 Aprili, 2020, imemwachia huru aliyekuwa Mbunge wa Ndanda kwa tiketi ya Chadema, Cecil Mwambe katika kesi ya uchochezi namba 263 ya mwaka 2017 iliyokuwa inamkabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara … (endelea).

Katika kesi hiyo Mwambe alishitakiwa kwa makosa mawili, kosa la kwanza, kutoa kauli za uchochezi alizotoa katika Kata Reli, wilaya Masasi, huku kosa la pili ni kufanya njama ya kutaka kutenda ovu.

Hakimu Kabate R. ametoa uamuzi huo wa kumwachia huru Mwambe, baada ya upande wa mashataka kushindwa kuthibitisha pasipo shaka kuwa mtuhumiwa alitenda makosa hayo, ambayo pia hayakuleta athari yoyote kwa jamii husika.

Mwambe alifunguliwa kesi hiyo akiwa Mbunge wa Ndanda kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) lakini alijivua uanachama wa chama hicho na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!