Thursday , 7 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama Mtwara yamwachia huru Mwambe
Habari za Siasa

Mahakama Mtwara yamwachia huru Mwambe

Spread the love

MAHAKAMA ya Mkoa wa Mtwara leo tarehe 30 Aprili, 2020, imemwachia huru aliyekuwa Mbunge wa Ndanda kwa tiketi ya Chadema, Cecil Mwambe katika kesi ya uchochezi namba 263 ya mwaka 2017 iliyokuwa inamkabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara … (endelea).

Katika kesi hiyo Mwambe alishitakiwa kwa makosa mawili, kosa la kwanza, kutoa kauli za uchochezi alizotoa katika Kata Reli, wilaya Masasi, huku kosa la pili ni kufanya njama ya kutaka kutenda ovu.

Hakimu Kabate R. ametoa uamuzi huo wa kumwachia huru Mwambe, baada ya upande wa mashataka kushindwa kuthibitisha pasipo shaka kuwa mtuhumiwa alitenda makosa hayo, ambayo pia hayakuleta athari yoyote kwa jamii husika.

Mwambe alifunguliwa kesi hiyo akiwa Mbunge wa Ndanda kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) lakini alijivua uanachama wa chama hicho na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bashungwa: Katesh kutafanyiwa usafi wa hali ya juu

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema kazi ya kuondoa tope...

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

error: Content is protected !!