Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya Iringa njia panda, mahakama yamtosa
Habari za Siasa

Meya Iringa njia panda, mahakama yamtosa

Alex Kimbe, Meya wa Manispaa ya Iringa
Spread the love

MAHAKAMA ya Mkoa wa Iringa, imetupilia mbali ombi la Alex Kimbe, Meya wa Manispaa ya Iringa la kuzuia mchakato wa kumng’oa madarakani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa…(endelea).

Uamuzi huo umetolewa leo tarehe 27 Machi 2020 na mahakama hiyo mbele ya Aden Kanje, Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Kanje amesema, ombi hilo limetupwa kutokana na kuwa na makosa, kitendo kilichopelekea mahakama hiyo kushindwa kusikiliza kesi hiyo kwa mujibu wa sheria.

Awali kikao cha kuendesha mchakato wa kumng’oa Meya Kimbe jana tarehe 26 Machi 2020, kilikwama baada ya madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutohudhuria.

Hata hivyo, Hamid Njovu, Mkurugenzi wa Halmshauri ya Manispaa ya Iringa, ameitisha Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani la manispaa hiyo, kesho tarehe 28 Machi 2020.

Miongoni mwa ajenda ya kikao hicho kesho, ni kupiga kura ya kutokuwa na imani na Meya Kimbe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!